... helping you be all that God made you to be, because He plans on shining His light into this world through you.

Berni - ceo, Christianityworks

Ni Kazi au ni Tukio Lisilo la Kawaida?

We're glad you like it!

Enjoying the content? You can save this to your favorites by logging in to your account.

Register or Login

Add to Favourites

Mathayo 4:18-20 Naye alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya, aliona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi. Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu. Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.

Listen to the radio broadcast of

Ni Kazi au ni Tukio Lisilo la Kawaida?


Download audio file

Niambie, unajishughulisha na nini siku baada ya siku?  Labda umeajiriwa, kwa hiyo unaenda kazini, Pengine wewe unatunza nyumba.  Au umestaafu , ni yapi yatachukua muda mwingi mwaka huu mpya?

Nikijibu swali langu mimi mwenyewe ni kwamba, nina  kazi, ila singesema ni “kazi” kama kazi.  Ni kweli, naenda “kazini” na ninaweza kushinda huko masaa mengi, lakini tangu nilipomfuata Yesu, ni kama sijafanya kazi. Sijui wewe ikoje? 

Ni kweli kwamba si kila mtu aliyeitwa anafanya kazi ya huduma muda wake wote.  Lakini kwa upande mwingine, kila mtu anayemwamini Yesu, maisha yake yamekusudiwa kuwa kama huduma wa milele ; haijalishi ajira yako ni ipi. 

Hilo ndilo lilikuwa lengo lake Yesu wakati aliwaambia jamaa hawa maneno yafuatayo: 

Mathayo 4:18-20  Naye alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya, aliona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi.  Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.  Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata. 

Aliwaondoa kwenye kazi ya kuvua samaki ili wawe wavuvi wa watu.  Ina maana alikuwa anawaongoza watumia vipawa na vipawa vyao kuwaambia watu wengine Habari Njema za Yesu.  Kweli hiyo ni shughuli isiyo ya kawaida. 

Kuna mtu mmoja aliwahi kusema hivi, ajira itajaza mfuko wako lakini kujishughulisha na matukio yasiyo ya kawaida kutajaza nafsi yako.  Kufuata wito wa Yesu kwenye maisha yako na kutumia vipawa na vipaji vyako ili uwaambie wengine habari za Yesu ni maisha yenye matukio ya ajabu.  Je!  Uko tayari? 

Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.