... helping you be all that God made you to be, because He plans on shining His light into this world through you.

Berni - ceo, Christianityworks

Kikomo cha Safari Yako

We're glad you like it!

Enjoying the content? You can save this to your favorites by logging in to your account.

Register or Login

Add to Favourites

1 Wakorintho 15:35,36 Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani? Ewe mpumbavu! Uipandayo haihuiki, isipokufa.

Listen to the radio broadcast of

Kikomo cha Safari Yako


Download audio file

Katika maisha ya kila siku kuna miangaiko mingi, fadhaa nyingi, mivutano na misongamano ya mambo tunayokutana nayo.  Lakini hata kama hayo yote yanatusumbua na kutawala mawazo yetu, siku moja … yote yataisha.

Sasa hatima yako inategemeana  na uamuzi wako kuweka tumaini lako kwaYesu au la!

Sasa, wengi wetu tunafahamu kwamba Yesu aliahidi uzima wa milele kwa wale watakaomwamini.  Lakini wewe na mimi, tumewapoteza rafiki na wapendwa wetu na kushiriki mazishi yao. 

Kwahiyo, hata kama huamini habari ya “uzima wa milele” ki-mantiki ni sawa ila tukisema ukweli, bado ni vigumu sana kukubari katika fikra zetu. 

Tunajua kwamba mtu anapokuwa amekufa mwili wake utaoza, baadhi ya Mila na Desturi huchoma mwili moto na kubaki na Majivu tu. Swala nzima la ufufuo na uzima wa milele, ki-utendaji linakuaje?  Mtume Paulo alijubu swali letu waziwazi 

1 Wakorintho 15:35,36  Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu?  Nao huja kwa mwili gani?  Ewe mpumbavu!  Uipandayo haihuiki, isipokufa. 

Alitumia mfano mzuri – dhana ya mbegu inayoonekana kwamba imekufa lakini hatimaye inahuiki na kumea.  Tutachunguza hiyo kesho.  Lakini kwa leo, tulijue hili angalau.  Kama unamwamini Yesu, jeneza ile si kikomo cha safari yako. 

Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.