... helping you be all that God made you to be, because He plans on shining His light into this world through you.

Berni - ceo, Christianityworks

Upumbavu wa Ukaidi

We're glad you like it!

Enjoying the content? You can save this to your favorites by logging in to your account.

Register or Login

Add to Favourites

Kumbukumbu 1:43-46 Basi niliwaambia, msinisikize, bali mliasi amri ya BWANA, mkajikinai, na kukwea mlimani. Na Waamori waliokuwa wakikaa katika mlima huo, waliwatokea juu yenu, wakawafukuza, kama wafukuzwao na nyuki, wakawapomoshea Seiri mpaka Horma. Mkarudi mkalia mbele za BWANA; BWANA asiisikize sauti yenu, wala hakuelekeza masikio yake kwenu. Ndipo mkakaa Kadeshi siku nyingi, kwa kadiri ya hizo siku mlizokaa.

Listen to the radio broadcast of

Upumbavu wa Ukaidi


Download audio file

Ni lini uliwahi kukutana na mtu mkaidi aliyekataa kusikiliza ushauri mzuri, mtu aliyekataa kunyenyekea hata kama alikuwa anaelekea pabaya, sema ukweli, ulipendezwa na mtu huyo!? 

Watu wenye ukaidi hawapendezi kabisa – ila kwa kusema ukweli sisi sote tunaweza kuwa wakaidi mara kwa mara. Tukio fulani linatushitua halafu tunajikuta kwenye msimamo sugu, tukiwa kinyume cha kila mtu – hata Mungu mwenyewe. 

Sasa, mtu akitulia kidogo na kutafakari, ataona kwamba kuwa mkaidi ni upumbavu. Kwani, kung’ang’ania ukaidi kumewahi kukusaidia kweli? 

Sikiliza Musa alivyoongea na taifa la Israeli walipoonyesha hali ya ukaidi. 

Kumbukumbu 1:43-46  Basi niliwaambia, msinisikize, bali mliasi amri ya BWANA, mkajikinai, na kukwea mlimani.  Na Waamori waliokuwa wakikaa katika mlima huo, waliwatokea juu yenu, wakawafukuza, kama wafukuzwao na nyuki, wakawapomoshea Seiri mpaka Horma.  Mkarudi mkalia mbele za BWANA; BWANA asiisikize sauti yenu, wala hakuelekeza masikio yake kwenu.  Ndipo mkakaa Kadeshi siku nyingi, kwa kadiri ya hizo siku mlizokaa. 

Walikataa kata kata kutii amri ya Bwana.  Badala ya kutii, wakapanda na ukaidi wao na kupigana na Waamori na mwishowe walishindwa kabisa – watu wakafa bure, vitu vikaharibika.

Kumbukumbu:  Wakati tunamuasi Mungu, tusitazamie kwamba atatusaidia pale mambo yatakapotuharibikia.  

Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.