... helping you be all that God made you to be, because He plans on shining His light into this world through you.

Berni - ceo, Christianityworks

Lengo la Ushindi

We're glad you like it!

Enjoying the content? You can save this to your favorites by logging in to your account.

Register or Login

Add to Favourites

2 Wakorintho 2:14-16 Ila Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza daima katika Kristo, na kuidhihirisha harufu ya kumjua yeye kila mahali kwa kazi yetu. Kwa maana sisi tu manukato ya Kristo, mbele za Mungu, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea; katika hao wa pili harufu ya mauti iletayo mauti; katika hao wa kwanza harufu ya uzima iletayo uzima. Naye ni nani atoshaye kwa mambo hayo?

Listen to the radio broadcast of

Lengo la Ushindi


Download audio file

Sote tunapenda neno “ushindi” neno hili linanahusu – mafanikio, utukufu, umaarufu, Ni nani asiyetaka kuishi maisha ya ushindi, akisongambele licha ya vipingamizi hadi kutokezea upande wa wake?

Kwahiyo, mtu akiazimia kuishi maisha ya ushindi ambayo Mungu ametuahidi kupitia Yesu Kristo, ni rahisi kukosea.  Kwasababu, mtu akiangalia kwa mtazamo wa ulimwengu, atafikiri kwamba ushindi wa Mungu unafanana na mafanikio ambayo ulimwengu unatuhakikishiakuwa ni haki yetu. 

Eeh, ni haki yako kabisa!  Umejitahidi sana!

Huo ndo wimbo wa wafanyabiashara wanaotushawishi tununue bidhaa zao,  Lakini sivyo Mungu anavyoeleza kuhusu habari za ushindi tulio nao katika Kristo. 

2 Wakorintho 2:14-16  Ila Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza daima katika Kristo, na kuidhihirisha harufu ya kumjua yeye kila mahali kwa kazi yetu.  Kwa maana sisi tu manukato ya Kristo, mbele za Mungu, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea; katika hao wa pili harufu ya mauti iletayo mauti; katika hao wa kwanza harufu ya uzima iletayo uzima.  Naye ni nani atoshaye kwa mambo hayo? 

Lengo la ushindi wa Kristo maishani mwetu si kwamba tuwe washindi na maarufu, bali ni kusudi tuonyeshe ulimwengu huu jinsi alivyo Yesu kwa njia ya ajabu kupitia kujitolea kwetu na unyenyekevu wetu.  Ni kweli, sio watapendezwa. Kuna wengine maneno hayo ni kama harufu ya manukato, na wengine ni kama harufu mbaya.  Lakini kwa vyovyote vile, endelea kuishia ushindi wa Yesu wenye unyenyekevu. 

Hili ndilo Neno la Mungu safi na lenye afya kwa ajili yako leo.